Wednesday, June 3, 2015

Paka mwenye umri mkubwa zaidi duniani afariki dunia

Paka huyo alievunja Rekodi ya Dunia kwa kuwa na umri mkubwa zaidi wa miaka 27 akiitwa 'Tiffany Two' amekufa akiwa kwenye usingizi.

Kifo chake kimewashtusha wapenzi wa wanyama wa kufugwa nyumbani nchini Marekani ambapo kitabu cha Rekodi za dunia Guiness Book kimeweka kumbukumbu kuwa Paka huyo mwenye umri wa miaka 27 alizaliwa
Machi 13, 1988, huko  San Diego, California, Marekani.

Paka huyo alinunuliwa na mmiliki wake Sharon Voorhees kutoka kwenye duka la wanyama wa kufugwa akiwa na umri wa wiki sita.

Sharon alimnunua paka huyo kwa Dola za Marekani 10$ sawa na shilingi 21,000 za Tanzania.
 
Umri wa kadri wa paka ni miaka 12 hadi 15.
 
Marehemu paka Tiffany Two alievunja rekodi ya dunia kama paka mwenye umri mkubwa zaidi. Amekufa akiwa ni umri wa miaka 27.

Marehemu paka Tiffany Two alievunja rekodi ya dunia kama paka mwenye umri mkubwa zaidi. Amekufa akiwa ni umri wa miaka 27.

Mama Sharon Voorhees aliefiwa na paka wake mkongwe, nadhani yu na majonzi kwa sasa.

No comments:

Post a Comment