Saturday, February 2, 2013

TAARIFA YA AJALI KUTOKA JESHI LA POLISI MBEYA



Taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa mbeya kwa vyombo vya habari
“press release” tarehe 02. 02.2013.

Wilaya ya mbarali - muendelezo wa taarifa ya ajali ya gari kupinduka na  
                                          Kusababisha vifo na majeruhi.

 Mnamo tarehe 01/02/2013 majira ya saa 07:15hrs huko kapunga chimala wilaya ya mbarali mkoa wa mbeya.

 Gari namba t.398 bse scania tipper 114 model mali ya mwekezaji aitwaye kapunga rice project likiendeshwa na dereva aitwaye baraka s/o mollel , miaka 29,mmasai na mkazi wa matebete likiwa limebeba vibarua wa kupanda mpunga kutoka kijiji cha mapogoro kwenda katika shamba la mwekezaji .

 Gari hilo likiwa ndani ya shamba hilo liliacha njia na kupinduka kisha kusababisha vifo vya watu wanne [4] ambao ni   1. Samweli s/o mapugilo, mbena, 30yrs na mkazi wa ilembula 2. Bon s/o mfupa, mnyakyusa, 27 yrs mkazi wa mapogolo na 3. Edgar s/o mwakipesile, miaka 35, kyusa, mkulima mkazi wa nonde mbeya na 4. Tazama s/o kazembe,miaka 34,msafwa,mkulima mkazi wa mswiwsi ambaye amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu hospitali ya rufaa mbeya. Aidha   katika ajali hiyo watu 130 walijeruhiwa kati yao wanaume 89 na wanawake 41. Majeruhi 74 kati yao wanaume 49 na wanawake 25 walipelekwa hospitali ya misheni chimala kwa ajili ya matibabu ambapo majeruhi 44 walipatiwa matibabu na kuruhusiwa na majeruhi 30 kati yao wanawake 14 na wanaume 16 wamelazwa hospitalini hapo wakiendelea kupatiwa matibabu. Aidha majeruhi wengine 56 waliopelekwa hospitali ya rufaa mbeya 22 walipatiwa matibabu na kuruhusiwa na majeruhi 34 wamelazwa hospitali hapo kwa matibabu zaidi kati yao wanawake 8 na wanaume 26 .

Mpaka sasa jumla ya majeruhi 64 bado wamelazwa katika hospitali za rufaa mbeya na chimala misheni hali zao zinaendelea vizuri na majeruhi 66 walipatiwa matibabu katika hospitali hizo na kuruhusiwa.

Chanzo cha ajali ni mwendo kasi uliosababishwa na vibarua waliokuwa ndani ya gari hilo kumshangilia dereva na gari  lilipofika kwenye kona lilimshinda kukata kona na kupinduka.  Dereva alikimbia mara baada ya tukio.  Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidizi wa polisi diwani athumani anatoa wito kwa madereva kuwa makini wanapokuwa barabarani kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.

 Aidha anatoa wito kwa mtu/watu wenye taarifa mahali alipo dereva azitoe ili akamatwe vinginevyo ajisalimishe mara moja. Pia anaendelea kuwaasa wananchi kuacha tabia ya kuwashabikia madereva wanaoendesha vyombo vya moto kwa mwendo kasi kwani inaweza kuhatarisha maisha na mali zao.



Signed by,
[diwani athumani – acp]
Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya.

No comments:

Post a Comment